Isaiah 22:12-14


12 aBwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,
aliwaita siku ile
ili kulia na kuomboleza,
kung’oa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.

13 bLakini tazama, kuna furaha na sherehe,
kuchinja ng’ombe na kuchinja kondoo,
kula nyama na kunywa mvinyo!
Mnasema, “Tuleni na kunywa,
kwa kuwa kesho tutakufa!”

14 c Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”

Copyright information for SwhKC